Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Judge

91 mistari · 6 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.

  2. Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.

  3. Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.

  4. Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.

  5. Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.

  6. Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.

  7. “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki na kuonyesha upendeleo kwa waovu?

  8. Teteeni wanyonge na yatima, tunzeni haki za maskini na walioonewa.

  9. Mwokoeni mnyonge na mhitaji, wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.

  10. Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,

  11. wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.

  12. Katika siku ile, Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuwa taji la utukufu, taji zuri la maua kwa mabaki ya watu wake.

  13. Atakuwa roho ya haki kwa yeye aketiye katika kiti cha hukumu, chanzo cha nguvu kwa wale wazuiao vita langoni.

  14. Watawafundisha watu wangu tofauti kati ya vitu vitakatifu na vitu vya kawaida na kuwaonyesha jinsi ya kupambanua kati ya vitu najisi na vitu safi.

  15. “ ‘Katika magombano yoyote, makuhani watatumika kama mahakimu na kuamua hilo jambo kufuatana na sheria zangu. Watazishika sheria zangu na maagizo yangu katika sikukuu zangu zote zilizoamriwa, nao watatakasa Sabato zangu.

  16. Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.

  17. Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.

  18. Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.

  19. Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo

  20. na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’ ”

  21. Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”

  22. Wakati huo Yesu akiwa amesimama mbele ya mtawala, mtawala akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.”

  23. Lakini viongozi wa makuhani na wazee walipomshtaki, hakujibu neno.

  24. Ndipo Pilato akamuuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi wanayokushtaki nayo?”

  25. Lakini Yesu hakumjibu hata kwa shtaka moja, kiasi kwamba mtawala alishangaa sana.