Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Integrity

96 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,

  2. basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.

  3. Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.

  4. “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’

  5. kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,

  6. kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,

  7. hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,

  8. basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.

  9. “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,

  10. lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;

  11. kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’

  12. Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;

  13. kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,

  14. kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:

  15. (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.

  16. Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.

  17. Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)

  18. “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,

  19. kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,

  20. basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

  21. Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya na kuna hatia mikononi mwangu,

  22. au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,

  23. basi adui anifuatie na kunipata, auponde uhai wangu ardhini na kunilaza mavumbini.

  24. Zaburi ya Daudi. Bwana, ni nani awezaye kukaa katika Hekalu lako? Nani awezaye kuishi katika mlima wako mtakatifu?

  25. Ni yule aendaye pasipo mawaa, atendaye yaliyo haki, asemaye kweli toka moyoni mwake,