Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Marko 14:66takriban 33 BK

    Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.

  2. Marko 14:67takriban 33 BK

    Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”

  3. Marko 14:68takriban 33 BK

    Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.

  4. Marko 14:69takriban 33 BK

    Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”

  5. Marko 14:70takriban 33 BK

    Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”

  6. Marko 14:71takriban 33 BK

    Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”

  7. Marko 14:72takriban 33 BK

    Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.

  8. Marko 15:1takriban 33 BK

    Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.

  9. Marko 15:2takriban 33 BK

    Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”

  10. Marko 15:3takriban 33 BK

    Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.

  11. Marko 15:4takriban 33 BK

    Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”

  12. Marko 15:5takriban 33 BK

    Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.

  13. Marko 15:6takriban 33 BK

    Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.

  14. Marko 15:7takriban 33 BK

    Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.

  15. Marko 15:8takriban 33 BK

    Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.

  16. Marko 15:9takriban 33 BK

    Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”

  17. Marko 15:10takriban 33 BK

    Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.

  18. Marko 15:11takriban 33 BK

    Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.

  19. Marko 15:12takriban 33 BK

    Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”

  20. Marko 15:13takriban 33 BK

    Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”

  21. Marko 15:14takriban 33 BK

    Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”

  22. Marko 15:15takriban 33 BK

    Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.

  23. Marko 15:16takriban 33 BK

    Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.

  24. Marko 15:17takriban 33 BK

    Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.

  25. Marko 15:18takriban 33 BK

    Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”