circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Marko 14:16takriban 33 BK
Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
- Marko 14:17takriban 33 BK
Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
- Marko 14:18takriban 33 BK
Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
- Marko 14:19takriban 33 BK
Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
- Marko 14:20takriban 33 BK
Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
- Marko 14:21takriban 33 BK
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
- Marko 14:22takriban 33 BK
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
- Marko 14:23takriban 33 BK
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
- Marko 14:24takriban 33 BK
Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
- Marko 14:25takriban 33 BK
Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
- Marko 14:26takriban 33 BK
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
- Marko 14:27takriban 33 BK
Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “ ‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
- Marko 14:28takriban 33 BK
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
- Marko 14:29takriban 33 BK
Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
- Marko 14:30takriban 33 BK
Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
- Marko 14:31takriban 33 BK
Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
- Marko 14:32takriban 33 BK
Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
- Marko 14:33takriban 33 BK
Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
- Marko 14:34takriban 33 BK
Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
- Marko 14:35takriban 33 BK
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
- Marko 14:36takriban 33 BK
Akasema, “Abba,Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
- Marko 14:37takriban 33 BK
Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
- Marko 14:38takriban 33 BK
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
- Marko 14:39takriban 33 BK
Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
- Marko 14:40takriban 33 BK
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.