Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Marko 13:3takriban 33 BK

    Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani,

  2. Marko 13:4takriban 33 BK

    “Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”

  3. Marko 13:5takriban 33 BK

    Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye.

  4. Marko 13:6takriban 33 BK

    Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi.

  5. Marko 13:7takriban 33 BK

    Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado.

  6. Marko 13:8takriban 33 BK

    Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

  7. Marko 13:9takriban 33 BK

    “Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao.

  8. Marko 13:10takriban 33 BK

    Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia.

  9. Marko 13:11takriban 33 BK

    Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.

  10. Marko 13:12takriban 33 BK

    “Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe.

  11. Marko 13:13takriban 33 BK

    Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

  12. Marko 13:14takriban 33 BK

    “Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.

  13. Marko 13:15takriban 33 BK

    Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote.

  14. Marko 13:16takriban 33 BK

    Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.

  15. Marko 13:17takriban 33 BK

    Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!

  16. Marko 13:18takriban 33 BK

    Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi.

  17. Marko 13:19takriban 33 BK

    Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe.

  18. Marko 13:20takriban 33 BK

    Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo.

  19. Marko 13:21takriban 33 BK

    Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristohuyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki.

  20. Marko 13:22takriban 33 BK

    Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule.

  21. Marko 13:23takriban 33 BK

    Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

  22. Marko 13:24takriban 33 BK

    “Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki, “ ‘jua litatiwa giza nao mwezi hautatoa nuru yake;

  23. Marko 13:25takriban 33 BK

    nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’

  24. Marko 13:26takriban 33 BK

    “Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu.

  25. Marko 13:27takriban 33 BK

    Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.