Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Marko 14:41takriban 33 BK

    Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.

  2. Marko 14:42takriban 33 BK

    Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”

  3. Marko 14:43takriban 33 BK

    Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.

  4. Marko 14:44takriban 33 BK

    Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”

  5. Marko 14:45takriban 33 BK

    Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.

  6. Marko 14:46takriban 33 BK

    Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.

  7. Marko 14:47takriban 33 BK

    Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.

  8. Marko 14:48takriban 33 BK

    Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?

  9. Marko 14:49takriban 33 BK

    Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”

  10. Marko 14:50takriban 33 BK

    Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.

  11. Marko 14:51takriban 33 BK

    Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,

  12. Marko 14:52takriban 33 BK

    alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.

  13. Marko 14:53takriban 33 BK

    Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.

  14. Marko 14:54takriban 33 BK

    Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.

  15. Marko 14:55takriban 33 BK

    Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.

  16. Marko 14:56takriban 33 BK

    Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.

  17. Marko 14:57takriban 33 BK

    Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:

  18. Marko 14:58takriban 33 BK

    “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’ ”

  19. Marko 14:59takriban 33 BK

    Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.

  20. Marko 14:60takriban 33 BK

    Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”

  21. Marko 14:61takriban 33 BK

    Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”

  22. Marko 14:62takriban 33 BK

    Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”

  23. Marko 14:63takriban 33 BK

    Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?

  24. Marko 14:64takriban 33 BK

    Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.

  25. Marko 14:65takriban 33 BK

    Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.