circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Marko 8:20takriban 32 BK
“Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Saba.”
- Marko 8:21takriban 32 BK
Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
- Marko 8:22takriban 32 BK
Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse.
- Marko 8:23takriban 32 BK
Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”
- Marko 8:24takriban 32 BK
Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
- Marko 8:25takriban 32 BK
Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
- Marko 8:26takriban 32 BK
Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”
- Marko 8:27takriban 32 BK
Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
- Marko 8:28takriban 32 BK
Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
- Marko 8:29takriban 32 BK
Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”
- Marko 8:30takriban 32 BK
Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
- Marko 8:31takriban 32 BK
Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke.
- Marko 8:32takriban 32 BK
Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
- Marko 8:33takriban 32 BK
Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
- Marko 8:34takriban 32 BK
Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
- Marko 8:35takriban 32 BK
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
- Marko 8:36takriban 32 BK
Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
- Marko 8:37takriban 32 BK
Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
- Marko 8:38takriban 32 BK
Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
- Marko 9:1takriban 32 BK
Yesu akaendelea kuwaambia, “Amin, nawaambia, kuna watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
- Marko 9:2takriban 32 BK
Baada ya siku sita, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao.
- Marko 9:3takriban 32 BK
Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko ambavyo mtu yeyote duniani angaliweza kuyangʼarisha.
- Marko 9:4takriban 32 BK
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Yesu.
- Marko 9:5takriban 32 BK
Petro akamwambia Yesu, “Rabi, ni vyema sisi tukae hapa. Turuhusu tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
- Marko 9:6takriban 32 BK
Petro hakujua aseme nini kwa maana yeye na wenzake walikuwa wameogopa sana.