circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Marko 7:32takriban 32 BK
Huko, watu wakamletea Yesu mtu mmoja kiziwi, ambaye pia alikuwa na kigugumizi, wakamwomba aweke mkono wake juu ya huyo mtu na amponye.
- Marko 7:33takriban 32 BK
Baadaye Yesu akampeleka yule kiziwi kando mbali na watu, Yesu akatia vidole vyake masikioni mwa yule mtu. Kisha akatema mate na kuugusa ulimi wa yule mtu.
- Marko 7:34takriban 32 BK
Ndipo Yesu akatazama mbinguni, akavuta hewa ndani kwa nguvu akamwambia, “Efatha!” (yaani, “Funguka!”)
- Marko 7:35takriban 32 BK
Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukaachiliwa, akaanza kuongea sawasawa.
- Marko 7:36takriban 32 BK
Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hizi. Lakini kadiri alivyowazuia, ndivyo walivyozidi kutangaza kwa bidii.
- Marko 7:37takriban 32 BK
Walistaajabu mno. Wakasema, “Amefanya mambo yote vizuri mno! Amewawezesha viziwi wasikie na bubu waseme!”
- Marko 8:1takriban 32 BK
Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
- Marko 8:2takriban 32 BK
“Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
- Marko 8:3takriban 32 BK
Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
- Marko 8:4takriban 32 BK
Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
- Marko 8:5takriban 32 BK
Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
- Marko 8:6takriban 32 BK
Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
- Marko 8:7takriban 32 BK
Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
- Marko 8:8takriban 32 BK
Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
- Marko 8:9takriban 32 BK
Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,
- Marko 8:10takriban 32 BK
aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
- Marko 8:11takriban 32 BK
Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
- Marko 8:12takriban 32 BK
Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
- Marko 8:13takriban 32 BK
Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.
- Marko 8:14takriban 32 BK
Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
- Marko 8:15takriban 32 BK
Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
- Marko 8:16takriban 32 BK
Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
- Marko 8:17takriban 32 BK
Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
- Marko 8:18takriban 32 BK
Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
- Marko 8:19takriban 32 BK
Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”