Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 23:10takriban 33 BK

    Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.

  2. Luka 23:11takriban 33 BK

    Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.

  3. Luka 23:12takriban 33 BK

    Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.

  4. Luka 23:13takriban 33 BK

    Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,

  5. Luka 23:14takriban 33 BK

    akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.

  6. Luka 23:15takriban 33 BK

    Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.

  7. Luka 23:16takriban 33 BK

    Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [

  8. Luka 23:17takriban 33 BK

    Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]

  9. Luka 23:18takriban 33 BK

    Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”

  10. Luka 23:19takriban 33 BK

    (Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)

  11. Luka 23:20takriban 33 BK

    Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.

  12. Luka 23:21takriban 33 BK

    Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”

  13. Luka 23:22takriban 33 BK

    Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”

  14. Luka 23:23takriban 33 BK

    Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.

  15. Luka 23:24takriban 33 BK

    Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.

  16. Luka 23:25takriban 33 BK

    Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.

  17. Luka 23:26takriban 33 BK

    Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.

  18. Luka 23:27takriban 33 BK

    Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.

  19. Luka 23:28takriban 33 BK

    Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.

  20. Luka 23:29takriban 33 BK

    Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’

  21. Luka 23:30takriban 33 BK

    Ndipo “ ‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!” ’

  22. Luka 23:31takriban 33 BK

    Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”

  23. Luka 23:32takriban 33 BK

    Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.

  24. Luka 23:33takriban 33 BK

    Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.

  25. Luka 23:34takriban 33 BK

    Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.