Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 22:56takriban 33 BK

    Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”

  2. Luka 22:57takriban 33 BK

    Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”

  3. Luka 22:58takriban 33 BK

    Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”

  4. Luka 22:59takriban 33 BK

    Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”

  5. Luka 22:60takriban 33 BK

    Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.

  6. Luka 22:61takriban 33 BK

    Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”

  7. Luka 22:62takriban 33 BK

    Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.

  8. Luka 22:63takriban 33 BK

    Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.

  9. Luka 22:64takriban 33 BK

    Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”

  10. Luka 22:65takriban 33 BK

    Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.

  11. Luka 22:66takriban 33 BK

    Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.

  12. Luka 22:67takriban 33 BK

    Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.

  13. Luka 22:68takriban 33 BK

    Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.

  14. Luka 22:69takriban 33 BK

    Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”

  15. Luka 22:70takriban 33 BK

    Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”

  16. Luka 22:71takriban 33 BK

    Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”

  17. Luka 23:1takriban 33 BK

    Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.

  18. Luka 23:2takriban 33 BK

    Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”

  19. Luka 23:3takriban 33 BK

    Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”

  20. Luka 23:4takriban 33 BK

    Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”

  21. Luka 23:5takriban 33 BK

    Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”

  22. Luka 23:6takriban 33 BK

    Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”

  23. Luka 23:7takriban 33 BK

    Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.

  24. Luka 23:8takriban 33 BK

    Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.

  25. Luka 23:9takriban 33 BK

    Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.