Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 22:6takriban 33 BK

    Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.

  2. Luka 22:7takriban 33 BK

    Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.

  3. Luka 22:8takriban 33 BK

    Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”

  4. Luka 22:9takriban 33 BK

    Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”

  5. Luka 22:10takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.

  6. Luka 22:11takriban 33 BK

    Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’

  7. Luka 22:12takriban 33 BK

    Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”

  8. Luka 22:13takriban 33 BK

    Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.

  9. Luka 22:14takriban 33 BK

    Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.

  10. Luka 22:15takriban 33 BK

    Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.

  11. Luka 22:16takriban 33 BK

    Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”

  12. Luka 22:17takriban 33 BK

    Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.

  13. Luka 22:18takriban 33 BK

    Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”

  14. Luka 22:19takriban 33 BK

    Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”

  15. Luka 22:20takriban 33 BK

    Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.

  16. Luka 22:21takriban 33 BK

    Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.

  17. Luka 22:22takriban 33 BK

    Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”

  18. Luka 22:23takriban 33 BK

    Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.

  19. Luka 22:24takriban 33 BK

    Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.

  20. Luka 22:25takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’

  21. Luka 22:26takriban 33 BK

    Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.

  22. Luka 22:27takriban 33 BK

    Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.

  23. Luka 22:28takriban 33 BK

    Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.

  24. Luka 22:29takriban 33 BK

    Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,

  25. Luka 22:30takriban 33 BK

    ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”