circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 22:6takriban 33 BK
Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
- Luka 22:7takriban 33 BK
Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
- Luka 22:8takriban 33 BK
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
- Luka 22:9takriban 33 BK
Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
- Luka 22:10takriban 33 BK
Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
- Luka 22:11takriban 33 BK
Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
- Luka 22:12takriban 33 BK
Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
- Luka 22:13takriban 33 BK
Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
- Luka 22:14takriban 33 BK
Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
- Luka 22:15takriban 33 BK
Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
- Luka 22:16takriban 33 BK
Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
- Luka 22:17takriban 33 BK
Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
- Luka 22:18takriban 33 BK
Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
- Luka 22:19takriban 33 BK
Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
- Luka 22:20takriban 33 BK
Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
- Luka 22:21takriban 33 BK
Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
- Luka 22:22takriban 33 BK
Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
- Luka 22:23takriban 33 BK
Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
- Luka 22:24takriban 33 BK
Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
- Luka 22:25takriban 33 BK
Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
- Luka 22:26takriban 33 BK
Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
- Luka 22:27takriban 33 BK
Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
- Luka 22:28takriban 33 BK
Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
- Luka 22:29takriban 33 BK
Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
- Luka 22:30takriban 33 BK
ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”