circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 23:35takriban 33 BK
Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
- Luka 23:36takriban 33 BK
Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
- Luka 23:37takriban 33 BK
na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
- Luka 23:38takriban 33 BK
Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
- Luka 23:39takriban 33 BK
Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
- Luka 23:40takriban 33 BK
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
- Luka 23:41takriban 33 BK
Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
- Luka 23:42takriban 33 BK
Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
- Luka 23:43takriban 33 BK
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
- Luka 23:44takriban 33 BK
Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
- Luka 23:45takriban 33 BK
kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
- Luka 23:46takriban 33 BK
Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
- Luka 23:47takriban 33 BK
Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
- Luka 23:48takriban 33 BK
Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
- Luka 23:49takriban 33 BK
Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
- Luka 23:50takriban 33 BK
Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
- Luka 23:51takriban 33 BK
lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
- Luka 23:52takriban 33 BK
Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
- Luka 23:53takriban 33 BK
Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
- Luka 23:54takriban 33 BK
Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
- Luka 23:55takriban 33 BK
Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
- Luka 23:56takriban 33 BK
Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.
- Luka 24:1takriban 33 BK
Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.
- Luka 24:2takriban 33 BK
Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,
- Luka 24:3takriban 33 BK
lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.