Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 23:35takriban 33 BK

    Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”

  2. Luka 23:36takriban 33 BK

    Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,

  3. Luka 23:37takriban 33 BK

    na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”

  4. Luka 23:38takriban 33 BK

    Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.

  5. Luka 23:39takriban 33 BK

    Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”

  6. Luka 23:40takriban 33 BK

    Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?

  7. Luka 23:41takriban 33 BK

    Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”

  8. Luka 23:42takriban 33 BK

    Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”

  9. Luka 23:43takriban 33 BK

    Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”

  10. Luka 23:44takriban 33 BK

    Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,

  11. Luka 23:45takriban 33 BK

    kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.

  12. Luka 23:46takriban 33 BK

    Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.

  13. Luka 23:47takriban 33 BK

    Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”

  14. Luka 23:48takriban 33 BK

    Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.

  15. Luka 23:49takriban 33 BK

    Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.

  16. Luka 23:50takriban 33 BK

    Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,

  17. Luka 23:51takriban 33 BK

    lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.

  18. Luka 23:52takriban 33 BK

    Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.

  19. Luka 23:53takriban 33 BK

    Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.

  20. Luka 23:54takriban 33 BK

    Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.

  21. Luka 23:55takriban 33 BK

    Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.

  22. Luka 23:56takriban 33 BK

    Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.

  23. Luka 24:1takriban 33 BK

    Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.

  24. Luka 24:2takriban 33 BK

    Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,

  25. Luka 24:3takriban 33 BK

    lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.