Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 24:4takriban 33 BK

    Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao.

  2. Luka 24:5takriban 33 BK

    Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?

  3. Luka 24:6takriban 33 BK

    Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:

  4. Luka 24:7takriban 33 BK

    ‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’ ”

  5. Luka 24:8takriban 33 BK

    Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.

  6. Luka 24:9takriban 33 BK

    Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote.

  7. Luka 24:10takriban 33 BK

    Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi.

  8. Luka 24:11takriban 33 BK

    Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.

  9. Luka 24:12takriban 33 BK

    Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.

  10. Luka 24:13takriban 33 BK

    Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba kutoka Yerusalemu.

  11. Luka 24:14takriban 33 BK

    Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia.

  12. Luka 24:15takriban 33 BK

    Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao,

  13. Luka 24:16takriban 33 BK

    lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.

  14. Luka 24:17takriban 33 BK

    Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?” Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni.

  15. Luka 24:18takriban 33 BK

    Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”

  16. Luka 24:19takriban 33 BK

    Akawauliza, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote.

  17. Luka 24:20takriban 33 BK

    Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha.

  18. Luka 24:21takriban 33 BK

    Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.

  19. Luka 24:22takriban 33 BK

    Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri,

  20. Luka 24:23takriban 33 BK

    lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai.

  21. Luka 24:24takriban 33 BK

    Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”

  22. Luka 24:25takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii!

  23. Luka 24:26takriban 33 BK

    Je, haikumpasa Kristokuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?”

  24. Luka 24:27takriban 33 BK

    Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.

  25. Luka 24:28takriban 33 BK

    Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele.