Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 24:29takriban 33 BK

    Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.

  2. Luka 24:30takriban 33 BK

    Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia.

  3. Luka 24:31takriban 33 BK

    Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena.

  4. Luka 24:32takriban 33 BK

    Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”

  5. Luka 24:33takriban 33 BK

    Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika

  6. Luka 24:34takriban 33 BK

    wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.”

  7. Luka 24:35takriban 33 BK

    Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.

  8. Luka 24:36takriban 33 BK

    Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”

  9. Luka 24:37takriban 33 BK

    Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.

  10. Luka 24:38takriban 33 BK

    Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?

  11. Luka 24:39takriban 33 BK

    Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”

  12. Luka 24:40takriban 33 BK

    Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.

  13. Luka 24:41takriban 33 BK

    Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”

  14. Luka 24:42takriban 33 BK

    Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,

  15. Luka 24:43takriban 33 BK

    naye akakichukua na kukila mbele yao.

  16. Luka 24:44takriban 33 BK

    Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”

  17. Luka 24:45takriban 33 BK

    Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.

  18. Luka 24:46takriban 33 BK

    Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu.

  19. Luka 24:47takriban 33 BK

    Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu.

  20. Luka 24:48takriban 33 BK

    Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.

  21. Luka 24:49takriban 33 BK

    “Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”

  22. Luka 24:50takriban 33 BK

    Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki.

  23. Luka 24:51takriban 33 BK

    Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni.

  24. Luka 24:52takriban 33 BK

    Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu.

  25. Luka 24:53takriban 33 BK

    Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.