circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 24:29takriban 33 BK
Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.
- Luka 24:30takriban 33 BK
Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia.
- Luka 24:31takriban 33 BK
Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena.
- Luka 24:32takriban 33 BK
Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”
- Luka 24:33takriban 33 BK
Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
- Luka 24:34takriban 33 BK
wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.”
- Luka 24:35takriban 33 BK
Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.
- Luka 24:36takriban 33 BK
Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
- Luka 24:37takriban 33 BK
Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.
- Luka 24:38takriban 33 BK
Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?
- Luka 24:39takriban 33 BK
Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
- Luka 24:40takriban 33 BK
Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
- Luka 24:41takriban 33 BK
Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
- Luka 24:42takriban 33 BK
Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
- Luka 24:43takriban 33 BK
naye akakichukua na kukila mbele yao.
- Luka 24:44takriban 33 BK
Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
- Luka 24:45takriban 33 BK
Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.
- Luka 24:46takriban 33 BK
Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu.
- Luka 24:47takriban 33 BK
Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu.
- Luka 24:48takriban 33 BK
Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
- Luka 24:49takriban 33 BK
“Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”
- Luka 24:50takriban 33 BK
Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki.
- Luka 24:51takriban 33 BK
Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni.
- Luka 24:52takriban 33 BK
Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu.
- Luka 24:53takriban 33 BK
Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.