Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 1:26takriban 5 BK

    Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.

  2. Yohana 1:27takriban 5 BK

    Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”

  3. Yohana 1:28takriban 5 BK

    Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.

  4. Yohana 1:29takriban 5 BK

    Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!

  5. Yohana 1:30takriban 5 BK

    Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’

  6. Yohana 1:31takriban 5 BK

    Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”

  7. Yohana 1:32takriban 5 BK

    Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.

  8. Yohana 1:33takriban 5 BK

    Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’

  9. Yohana 1:34takriban 5 BK

    Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”

  10. Yohana 1:35takriban 5 BK

    Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.

  11. Yohana 1:36takriban 5 BK

    Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”

  12. Yohana 1:37takriban 5 BK

    Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.

  13. Yohana 1:38takriban 5 BK

    Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”

  14. Yohana 1:39takriban 5 BK

    Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.

  15. Yohana 1:40takriban 5 BK

    Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.

  16. Yohana 1:41takriban 5 BK

    Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).

  17. Yohana 1:42takriban 5 BK

    Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).

  18. Yohana 1:43takriban 5 BK

    Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”

  19. Yohana 1:44takriban 5 BK

    Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.

  20. Yohana 1:45takriban 5 BK

    Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”

  21. Yohana 1:46takriban 5 BK

    Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”

  22. Yohana 1:47takriban 5 BK

    Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”

  23. Yohana 1:48takriban 5 BK

    Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”

  24. Yohana 1:49takriban 5 BK

    Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”

  25. Yohana 1:50takriban 5 BK

    Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”