Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 2:25takriban 4 KK

    Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.

  2. Yohana 3:1takriban 30 BK

    Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.

  3. Yohana 3:2takriban 30 BK

    Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”

  4. Yohana 3:3takriban 30 BK

    Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”

  5. Yohana 3:4takriban 30 BK

    Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”

  6. Yohana 3:5takriban 30 BK

    Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.

  7. Yohana 3:6takriban 30 BK

    Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.

  8. Yohana 3:7takriban 30 BK

    Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’

  9. Yohana 3:8takriban 30 BK

    Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”

  10. Yohana 3:9takriban 30 BK

    Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”

  11. Yohana 3:10takriban 30 BK

    Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?

  12. Yohana 3:11takriban 30 BK

    Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.

  13. Yohana 3:12takriban 30 BK

    Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?

  14. Yohana 3:13takriban 30 BK

    Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.

  15. Yohana 3:14takriban 30 BK

    Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.

  16. Yohana 3:15takriban 30 BK

    Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele.

  17. Yohana 3:16takriban 30 BK

    “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

  18. Yohana 3:17takriban 30 BK

    Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.

  19. Yohana 3:18takriban 30 BK

    Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

  20. Yohana 3:19takriban 30 BK

    Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.

  21. Yohana 3:20takriban 30 BK

    Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.

  22. Yohana 3:21takriban 30 BK

    Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”

  23. Yohana 3:22takriban 30 BK

    Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.

  24. Yohana 3:23takriban 30 BK

    Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.

  25. Yohana 3:24takriban 30 BK

    (Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).