Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 4:14takriban 30 BK

    Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.”

  2. Yohana 4:15takriban 30 BK

    Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”

  3. Yohana 4:16takriban 30 BK

    Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”

  4. Yohana 4:17takriban 30 BK

    Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.

  5. Yohana 4:18takriban 30 BK

    Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”

  6. Yohana 4:19takriban 30 BK

    Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.

  7. Yohana 4:20takriban 30 BK

    Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”

  8. Yohana 4:21takriban 30 BK

    Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.

  9. Yohana 4:22takriban 30 BK

    Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.

  10. Yohana 4:23takriban 30 BK

    Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.

  11. Yohana 4:24takriban 30 BK

    Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”

  12. Yohana 4:25takriban 30 BK

    Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”

  13. Yohana 4:26takriban 30 BK

    Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”

  14. Yohana 4:27takriban 30 BK

    Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”

  15. Yohana 4:28takriban 30 BK

    Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,

  16. Yohana 4:29takriban 30 BK

    “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”

  17. Yohana 4:30takriban 30 BK

    Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.

  18. Yohana 4:31takriban 30 BK

    Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”

  19. Yohana 4:32takriban 30 BK

    Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”

  20. Yohana 4:33takriban 30 BK

    Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”

  21. Yohana 4:34takriban 30 BK

    Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.

  22. Yohana 4:35takriban 30 BK

    Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!

  23. Yohana 4:36takriban 30 BK

    Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja.

  24. Yohana 4:37takriban 30 BK

    Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.

  25. Yohana 4:38takriban 30 BK

    Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”