Rukia maudhui

circa 1446 BC

Sinai & The Law

God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.

1,657 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kutoka 26:13takriban 1491 KK

    Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.

  2. Kutoka 26:14takriban 1491 KK

    Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.

  3. Kutoka 26:15takriban 1491 KK

    “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.

  4. Kutoka 26:16takriban 1491 KK

    Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,

  5. Kutoka 26:17takriban 1491 KK

    zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.

  6. Kutoka 26:18takriban 1491 KK

    Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,

  7. Kutoka 26:19takriban 1491 KK

    kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.

  8. Kutoka 26:20takriban 1491 KK

    Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini

  9. Kutoka 26:21takriban 1491 KK

    na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

  10. Kutoka 26:22takriban 1491 KK

    Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,

  11. Kutoka 26:23takriban 1491 KK

    na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.

  12. Kutoka 26:24takriban 1491 KK

    Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.

  13. Kutoka 26:25takriban 1491 KK

    Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

  14. Kutoka 26:26takriban 1491 KK

    “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,

  15. Kutoka 26:27takriban 1491 KK

    matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.

  16. Kutoka 26:28takriban 1491 KK

    Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.

  17. Kutoka 26:29takriban 1491 KK

    Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.

  18. Kutoka 26:30takriban 1491 KK

    “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

  19. Kutoka 26:31takriban 1491 KK

    “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.

  20. Kutoka 26:32takriban 1491 KK

    Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.

  21. Kutoka 26:33takriban 1491 KK

    Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.

  22. Kutoka 26:34takriban 1491 KK

    Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.

  23. Kutoka 26:35takriban 1491 KK

    Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.

  24. Kutoka 26:36takriban 1491 KK

    “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.

  25. Kutoka 26:37takriban 1491 KK

    Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.