Rukia maudhui

circa 1050–1010 BC

Samuel & King Saul

Israel demands a king; Samuel anoints Saul, whose disobedience leads to his rejection as God chooses a man after his own heart.

810 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. 1 Samweli 7:11takriban 1120 KK

    Watu wa Israeli wakatoka mbio huko Mispa na kuwafuatia Wafilisti, wakiwachinja njiani hadi mahali chini ya Beth-Kari.

  2. 1 Samweli 7:12takriban 1120 KK

    Ndipo Samweli akachukua jiwe na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni. Akaliita Ebenezeri, akisema, “Hata sasa Bwana ametusaidia.”

  3. 1 Samweli 7:13takriban 1120 KK

    Basi Wafilisti wakashindwa na hawakuvamia nchi ya Israeli tena. Katika maisha yote ya Samweli, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya Wafilisti.

  4. 1 Samweli 7:14takriban 1120 KK

    Miji kuanzia Ekroni hadi Gathi, ile ambayo Wafilisti walikuwa wameiteka kutoka Israeli, ilirudishwa kwake, naye Israeli akazikomboa nchi jirani mikononi mwa Wafilisti. Kukawepo amani kati ya Israeli na Waamori.

  5. 1 Samweli 7:15takriban 1131 KK

    Samweli akaendelea kama mwamuzi juu ya Israeli siku zote za maisha yake.

  6. 1 Samweli 7:16takriban 1131 KK

    Mwaka hadi mwaka aliendelea kuzunguka kutoka Betheli mpaka Gilgali na Mispa, akiamua Israeli katika sehemu hizo zote.

  7. 1 Samweli 7:17takriban 1131 KK

    Lakini kila mara alirudi Rama, kulikokuwa nyumbani kwake, huko pia aliwaamua Israeli. Naye huko alimjengea Bwana madhabahu.

  8. 1 Samweli 8:1takriban 1112 KK

    Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.

  9. 1 Samweli 8:2takriban 1112 KK

    Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.

  10. 1 Samweli 8:3takriban 1112 KK

    Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.

  11. 1 Samweli 8:4takriban 1112 KK

    Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.

  12. 1 Samweli 8:5takriban 1112 KK

    Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”

  13. 1 Samweli 8:6takriban 1112 KK

    Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.

  14. 1 Samweli 8:7takriban 1112 KK

    Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.

  15. 1 Samweli 8:8takriban 1112 KK

    Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.

  16. 1 Samweli 8:9takriban 1112 KK

    Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”

  17. 1 Samweli 8:10takriban 1112 KK

    Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.

  18. 1 Samweli 8:11takriban 1112 KK

    Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.

  19. 1 Samweli 8:12takriban 1112 KK

    Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.

  20. 1 Samweli 8:13takriban 1112 KK

    Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.

  21. 1 Samweli 8:14takriban 1112 KK

    Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.

  22. 1 Samweli 8:15takriban 1112 KK

    Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.

  23. 1 Samweli 8:16takriban 1112 KK

    Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.

  24. 1 Samweli 8:17takriban 1112 KK

    Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.

  25. 1 Samweli 8:18takriban 1112 KK

    Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”