Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Select Readings

802 mistari · 47 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.

  2. Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

  3. “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

  4. Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.

  5. Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.

  6. Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

  7. Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

  8. Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.

  9. Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

  10. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, Bwana wetu, tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Umeuweka utukufu wako juu ya mbingu.

  11. Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa, kwa sababu ya watesi wako, kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

  12. Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota, ulizoziratibisha,

  13. mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?

  14. Umemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni, ukamvika taji ya utukufu na heshima.

  15. Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako; umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.

  16. Mifugo na makundi yote pia, naam, na wanyama wa kondeni,

  17. ndege wa angani na samaki wa baharini, naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

  18. Ee Bwana, Bwana wetu, tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

  19. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.

  20. Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.

  21. Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.

  22. Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

  23. Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili.

  24. Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.

  25. Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.