Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Malice

135 mistari · 29 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.

  2. Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.

  3. Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.

  4. Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”

  5. Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.

  6. Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.

  7. Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.

  8. Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.

  9. Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu.

  10. Wale waniambiao, “Aha! Aha!” warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

  11. Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.

  12. Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”

  13. kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.

  14. Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.

  15. Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.

  16. Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.

  17. Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

  18. Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

  19. Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.

  20. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,

  21. ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.

  22. Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.

  23. Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.

  24. Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.

  25. Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.