Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Malice: General references

111 mistari · 29 vipengele

Mistari kuhusu General references

Chuja kwa kitabu
  1. “ ‘Usimchukie ndugu yako moyoni mwako. Karipia jirani yako kwa uwazi ili usishiriki hatia yake.

  2. “ ‘Usijilipizie kisasi wala kuwa na kinyongo dhidi ya mmoja wa jamaa yako, lakini mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ndimi Bwana.

  3. “Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”

  4. “Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”

  5. Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kutoka kwenye mashamba ya Gomora. Zabibu zake zimejaa sumu, na vishada vyake vimejaa uchungu.

  6. Mvinyo wao ni sumu ya nyoka, sumu yenye kufisha ya swila.

  7. Wakati mfalme wa Israeli alipowaona, akamuuliza Elisha, “Je, baba yangu, niwaue?”

  8. Naye akajibu, “Usiwaue. Je, utawaua watu uliowateka kwa upanga wako mwenyewe na upinde wako? Wape chakula na maji ili wapate kula na kunywa, na kisha wamrudie bwana wao.”

  9. “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,

  10. lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;

  11. Yeye aliye na mimba ya uovu na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.

  12. Yeye achimbaye shimo na kulifukua hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.

  13. Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.

  14. Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.

  15. Huvizia karibu na vijiji; kutoka mafichoni huwanasa wasio na hatia, akivizia wapitaji.

  16. Huvizia kama simba aliye mawindoni; huvizia kumkamata mnyonge, huwakamata wanyonge na kuwaburuza katika wavu wake.

  17. Mateka wake hupondwa, huzimia; wanaanguka katika nguvu zake.

  18. Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

  19. Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”

  20. Lakini nilipojikwaa, walikusanyika kwa shangwe; washambuliaji walijikusanya dhidi yangu bila mimi kujua. Walinisingizia pasipo kukoma.

  21. Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.

  22. Usiwaache wale wanaonisimanga, wale ambao ni adui zangu bila sababu; usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu wakonyeze jicho kwa hila.

  23. Hawazungumzi kwa amani, bali wanatunga mashtaka ya uongo dhidi ya wale wanaoishi kwa utulivu katika nchi.

  24. Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha! Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

  25. Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”