- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Idolatry
Mistari muhimu ya Biblia
Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
“Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, zina pua, lakini haziwezi kunusa;
zina mikono, lakini haziwezi kupapasa, zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala koo zao haziwezi kutoa sauti.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.