Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Answers To Prayer

195 mistari · 85 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,

  2. Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.

  3. Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?

  4. Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?

  5. Yeye hajibu wakati watu waliapo kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

  6. Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili; Mwenyezi hayazingatii.

  7. Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.

  8. Kwa maana yeye alipizaye kisasi cha damu hukumbuka, hapuuzi kilio cha wanaoonewa.

  9. Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.

  10. Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.

  11. Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.

  12. Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

  13. Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.

  14. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Nilimngoja Bwana kwa saburi, naye akaniinamia, akasikia kilio changu.

  15. na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”

  16. Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, Bwana asingekuwa amenisikiliza;

  17. Sifa apewe Mungu, ambaye hakulikataa ombi langu wala kunizuilia upendo wake!

  18. Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.

  19. Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.

  20. Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.

  21. Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;

  22. Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.

  23. Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.

  24. Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.

  25. Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.