- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Animals
Mistari muhimu ya Biblia
Ndipo Bwana akapeleka nyoka wenye sumu katikati yao; wakawauma watu, nao Waisraeli wengi wakafa.
Watu wakamjia Mose na kusema, “Tumetenda dhambi wakati tuliponena dhidi ya Bwana na dhidi yako. Mwombe Bwana ili atuondolee hawa nyoka.” Hivyo Mose akawaombea hao watu.
Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
kunguru wa aina yoyote,
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
bundi, mumbi, bundi mkubwa,
mwari, nderi, mnandi,
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.