Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Afflictions and Adversities

526 mistari · 5 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.

  2. Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.

  3. Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha;

  4. kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.

  5. Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.

  6. Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.

  7. Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.

  8. Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.

  9. Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.

  10. Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.

  11. Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

  12. Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

  13. Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.

  14. Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.

  15. Bwana huwategemeza wote waangukao, na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.

  16. Anawaponya waliovunjika mioyo na kuvifunga vidonda vyao.

  17. Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,

  18. kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.

  19. Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.

  20. Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.

  21. Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!

  22. Nikatazama tena nikaona uonevu wote uliokuwa unafanyika chini ya jua: Nikaona machozi ya walioonewa, wala hawana wa kuwafariji; uwezo ulikuwa upande wa wale wanaowaonea, wala hawana wa kuwafariji.

  23. Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.

  24. Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.

  25. Utakuwa sitara na kivuli kutokana na joto la mchana, na kuwa mahali pa kujificha kutokana na dhoruba na mvua.