circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 25:37takriban 33 BK
“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakulisha, au ukiwa na kiu tukakunywesha?
- Mathayo 25:38takriban 33 BK
Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha, au ukiwa uchi tukakuvika?
- Mathayo 25:39takriban 33 BK
Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza, au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’
- Mathayo 25:40takriban 33 BK
“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi mlivyomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.’
- Mathayo 25:41takriban 33 BK
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake.
- Mathayo 25:42takriban 33 BK
Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha,
- Mathayo 25:43takriban 33 BK
nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza, na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’
- Mathayo 25:44takriban 33 BK
“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’
- Mathayo 25:45takriban 33 BK
“Naye atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’
- Mathayo 25:46takriban 33 BK
“Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.”
- Mathayo 26:1takriban 33 BK
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
- Mathayo 26:2takriban 33 BK
“Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
- Mathayo 26:3takriban 33 BK
Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
- Mathayo 26:4takriban 33 BK
Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
- Mathayo 26:5takriban 33 BK
Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
- Mathayo 26:6takriban 33 BK
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
- Mathayo 26:7takriban 33 BK
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
- Mathayo 26:8takriban 33 BK
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
- Mathayo 26:9takriban 33 BK
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
- Mathayo 26:10takriban 33 BK
Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
- Mathayo 26:11takriban 33 BK
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
- Mathayo 26:12takriban 33 BK
Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
- Mathayo 26:13takriban 33 BK
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
- Mathayo 26:14takriban 33 BK
Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
- Mathayo 26:15takriban 33 BK
na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.