Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 25:37takriban 33 BK

    “Ndipo wale wenye haki watakapomjibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakulisha, au ukiwa na kiu tukakunywesha?

  2. Mathayo 25:38takriban 33 BK

    Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha, au ukiwa uchi tukakuvika?

  3. Mathayo 25:39takriban 33 BK

    Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza, au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’

  4. Mathayo 25:40takriban 33 BK

    “Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi mlivyomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.’

  5. Mathayo 25:41takriban 33 BK

    “Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake.

  6. Mathayo 25:42takriban 33 BK

    Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha,

  7. Mathayo 25:43takriban 33 BK

    nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza, na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’

  8. Mathayo 25:44takriban 33 BK

    “Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’

  9. Mathayo 25:45takriban 33 BK

    “Naye atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’

  10. Mathayo 25:46takriban 33 BK

    “Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.”

  11. Mathayo 26:1takriban 33 BK

    Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,

  12. Mathayo 26:2takriban 33 BK

    “Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”

  13. Mathayo 26:3takriban 33 BK

    Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.

  14. Mathayo 26:4takriban 33 BK

    Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.

  15. Mathayo 26:5takriban 33 BK

    Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”

  16. Mathayo 26:6takriban 33 BK

    Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,

  17. Mathayo 26:7takriban 33 BK

    naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.

  18. Mathayo 26:8takriban 33 BK

    Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?

  19. Mathayo 26:9takriban 33 BK

    Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”

  20. Mathayo 26:10takriban 33 BK

    Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.

  21. Mathayo 26:11takriban 33 BK

    Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.

  22. Mathayo 26:12takriban 33 BK

    Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.

  23. Mathayo 26:13takriban 33 BK

    Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”

  24. Mathayo 26:14takriban 33 BK

    Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani

  25. Mathayo 26:15takriban 33 BK

    na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.