Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 25:12takriban 33 BK

    “Lakini yeye bwana arusi akawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, siwajui ninyi!’

  2. Mathayo 25:13takriban 33 BK

    “Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa.

  3. Mathayo 25:14takriban 33 BK

    “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama mtu aliyetaka kusafiri, naye akawaita watumishi wake na kuweka mali yake kwenye uangalizi wao.

  4. Mathayo 25:15takriban 33 BK

    Mmoja akampa talantatano, mwingine talanta mbili, na mwingine talanta moja. Kila mmoja alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye akasafiri.

  5. Mathayo 25:16takriban 33 BK

    Yule aliyepewa talanta tano akaenda mara moja akafanya nazo biashara akapata talanta nyingine tano zaidi.

  6. Mathayo 25:17takriban 33 BK

    Yule aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo, akapata nyingine mbili zaidi.

  7. Mathayo 25:18takriban 33 BK

    Lakini yule mtumishi aliyekuwa amepokea talanta moja, alikwenda akachimba shimo ardhini na kuificha ile fedha ya bwana wake.

  8. Mathayo 25:19takriban 33 BK

    “Baada ya muda mrefu, yule bwana wa wale watumishi akarudi na kufanya hesabu nao.

  9. Mathayo 25:20takriban 33 BK

    Yule mtumishi aliyepokea talanta tano akaja, akaleta nyingine tano zaidi. Akasema, ‘Bwana uliweka kwenye uangalizi wangu talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta tano zaidi.’

  10. Mathayo 25:21takriban 33 BK

    “Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’

  11. Mathayo 25:22takriban 33 BK

    “Yule mwenye talanta mbili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, uliweka kwenye uangalizi wangu talanta mbili. Tazama nimepata hapa talanta mbili zaidi.’

  12. Mathayo 25:23takriban 33 BK

    “Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’

  13. Mathayo 25:24takriban 33 BK

    “Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu.

  14. Mathayo 25:25takriban 33 BK

    Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’

  15. Mathayo 25:26takriban 33 BK

    “Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu.

  16. Mathayo 25:27takriban 33 BK

    Vyema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, ili nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake.

  17. Mathayo 25:28takriban 33 BK

    “ ‘Basi mnyangʼanyeni hiyo talanta, mkampe yule mwenye talanta kumi.

  18. Mathayo 25:29takriban 33 BK

    Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.

  19. Mathayo 25:30takriban 33 BK

    Nanyi mtupeni huyo mtumishi asiyefaa nje, kwenye giza, mahali ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’

  20. Mathayo 25:31takriban 33 BK

    “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake.

  21. Mathayo 25:32takriban 33 BK

    Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.

  22. Mathayo 25:33takriban 33 BK

    Atawaweka kondoo upande wake wa kuume, na mbuzi upande wake wa kushoto.

  23. Mathayo 25:34takriban 33 BK

    “Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njooni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu; urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

  24. Mathayo 25:35takriban 33 BK

    Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha,

  25. Mathayo 25:36takriban 33 BK

    nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’