circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 24:38takriban 33 BK
Kwa maana siku zile kabla ya gharika, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina.
- Mathayo 24:39takriban 33 BK
Nao hawakujua lolote mpaka gharika ilipokuja ikawakumba wote. Hivyo ndivyo itakavyokuwa atakapokuja Mwana wa Adamu.
- Mathayo 24:40takriban 33 BK
Watu wawili watakuwa shambani, naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
- Mathayo 24:41takriban 33 BK
Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja, naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
- Mathayo 24:42takriban 33 BK
“Basi kesheni, kwa sababu hamjui ni siku gani atakapokuja Bwana wenu.
- Mathayo 24:43takriban 33 BK
Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua ni wakati gani wa usiku ambao mwizi atakuja, angekesha na hangekubali nyumba yake kuvunjwa.
- Mathayo 24:44takriban 33 BK
Kwa hiyo ninyi pia hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.
- Mathayo 24:45takriban 33 BK
“Ni nani basi aliye mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake amemweka kusimamia watumishi wengine katika nyumba yake, ili awape chakula chao kwa wakati unaofaa?
- Mathayo 24:46takriban 33 BK
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
- Mathayo 24:47takriban 33 BK
Amin, nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
- Mathayo 24:48takriban 33 BK
Lakini kama huyo mtumishi ni mwovu, naye akasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu atakawia muda mrefu,’
- Mathayo 24:49takriban 33 BK
kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, na kula na kunywa pamoja na walevi.
- Mathayo 24:50takriban 33 BK
Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua.
- Mathayo 24:51takriban 33 BK
Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wanafiki, mahali ambako kutakuwa ni kulia na kusaga meno.
- Mathayo 25:1takriban 33 BK
“Wakati huo, Ufalme wa Mbinguni utakuwa kama wanawali kumi waliochukua taa zao na kwenda kumlaki bwana arusi.
- Mathayo 25:2takriban 33 BK
Watano wao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
- Mathayo 25:3takriban 33 BK
Wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta ya akiba,
- Mathayo 25:4takriban 33 BK
lakini wale wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya akiba kwenye vyombo.
- Mathayo 25:5takriban 33 BK
Bwana arusi alipokawia kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala.
- Mathayo 25:6takriban 33 BK
“Usiku wa manane pakawa na kelele: ‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje mkamlaki!’
- Mathayo 25:7takriban 33 BK
“Ndipo wale wanawali wote wakaamka na kuzitengeneza taa zao.
- Mathayo 25:8takriban 33 BK
Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta yenu kidogo; taa zetu zinazimika.’
- Mathayo 25:9takriban 33 BK
“Lakini wale wenye busara wakawajibu, ‘Sivyo, hayatutoshi sisi na ninyi pia. Afadhali mwende kwa wauzao mkajinunulie mafuta yenu.’
- Mathayo 25:10takriban 33 BK
“Nao walipokuwa wakienda kununua mafuta, bwana arusi akafika. Wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia ndani pamoja naye kwenye karamu ya arusi na mlango ukafungwa.
- Mathayo 25:11takriban 33 BK
“Baadaye wale wanawali wengine nao wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mlango!’