circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 22:23takriban 33 BK
Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
- Mathayo 22:24takriban 33 BK
“Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
- Mathayo 22:25takriban 33 BK
Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
- Mathayo 22:26takriban 33 BK
Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
- Mathayo 22:27takriban 33 BK
Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
- Mathayo 22:28takriban 33 BK
Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
- Mathayo 22:29takriban 33 BK
Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
- Mathayo 22:30takriban 33 BK
Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
- Mathayo 22:31takriban 33 BK
Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
- Mathayo 22:32takriban 33 BK
‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
- Mathayo 22:33takriban 33 BK
Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
- Mathayo 22:34takriban 33 BK
Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
- Mathayo 22:35takriban 33 BK
Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
- Mathayo 22:36takriban 33 BK
“Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
- Mathayo 22:37takriban 33 BK
Yesu akamjibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
- Mathayo 22:38takriban 33 BK
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
- Mathayo 22:39takriban 33 BK
Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
- Mathayo 22:40takriban 33 BK
Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
- Mathayo 22:41takriban 33 BK
Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
- Mathayo 22:42takriban 33 BK
“Mnaonaje kuhusu Kristo?Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
- Mathayo 22:43takriban 33 BK
Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
- Mathayo 22:44takriban 33 BK
“ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.” ’
- Mathayo 22:45takriban 33 BK
Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
- Mathayo 22:46takriban 33 BK
Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.
- Mathayo 23:1takriban 33 BK
Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake: