Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 22:23takriban 33 BK

    Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,

  2. Mathayo 22:24takriban 33 BK

    “Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’

  3. Mathayo 22:25takriban 33 BK

    Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.

  4. Mathayo 22:26takriban 33 BK

    Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.

  5. Mathayo 22:27takriban 33 BK

    Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.

  6. Mathayo 22:28takriban 33 BK

    Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”

  7. Mathayo 22:29takriban 33 BK

    Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.

  8. Mathayo 22:30takriban 33 BK

    Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.

  9. Mathayo 22:31takriban 33 BK

    Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,

  10. Mathayo 22:32takriban 33 BK

    ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”

  11. Mathayo 22:33takriban 33 BK

    Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.

  12. Mathayo 22:34takriban 33 BK

    Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.

  13. Mathayo 22:35takriban 33 BK

    Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,

  14. Mathayo 22:36takriban 33 BK

    “Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”

  15. Mathayo 22:37takriban 33 BK

    Yesu akamjibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’

  16. Mathayo 22:38takriban 33 BK

    Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.

  17. Mathayo 22:39takriban 33 BK

    Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’

  18. Mathayo 22:40takriban 33 BK

    Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”

  19. Mathayo 22:41takriban 33 BK

    Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,

  20. Mathayo 22:42takriban 33 BK

    “Mnaonaje kuhusu Kristo?Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”

  21. Mathayo 22:43takriban 33 BK

    Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,

  22. Mathayo 22:44takriban 33 BK

    “ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.” ’

  23. Mathayo 22:45takriban 33 BK

    Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”

  24. Mathayo 22:46takriban 33 BK

    Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.

  25. Mathayo 23:1takriban 33 BK

    Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake: