circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 21:44takriban 33 BK
Yeye aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
- Mathayo 21:45takriban 33 BK
Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao.
- Mathayo 21:46takriban 33 BK
Wakatafuta njia ya kumkamata, lakini wakaogopa umati wa watu, kwa kuwa watu walimwona Yesu kuwa ni nabii.
- Mathayo 22:1takriban 33 BK
Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
- Mathayo 22:2takriban 33 BK
“Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
- Mathayo 22:3takriban 33 BK
Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
- Mathayo 22:4takriban 33 BK
“Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
- Mathayo 22:5takriban 33 BK
“Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
- Mathayo 22:6takriban 33 BK
Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
- Mathayo 22:7takriban 33 BK
Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
- Mathayo 22:8takriban 33 BK
“Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
- Mathayo 22:9takriban 33 BK
Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
- Mathayo 22:10takriban 33 BK
Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
- Mathayo 22:11takriban 33 BK
“Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
- Mathayo 22:12takriban 33 BK
Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
- Mathayo 22:13takriban 33 BK
“Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
- Mathayo 22:14takriban 33 BK
“Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
- Mathayo 22:15takriban 33 BK
Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
- Mathayo 22:16takriban 33 BK
Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
- Mathayo 22:17takriban 33 BK
Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
- Mathayo 22:18takriban 33 BK
Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
- Mathayo 22:19takriban 33 BK
Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
- Mathayo 22:20takriban 33 BK
Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
- Mathayo 22:21takriban 33 BK
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
- Mathayo 22:22takriban 33 BK
Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.