Rukia maudhui

circa 800–400 BC

The Hebrew Prophets

God speaks through Isaiah, Jeremiah, and the minor prophets—calling Israel to repentance and foretelling the coming Messiah.

3,706 mistari · 14 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hosea 10:14takriban 740 KK

    mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.

  2. Hosea 10:15takriban 740 KK

    Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.

  3. Hosea 11:1takriban 740 KK

    “Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda, nilimwita mwanangu kutoka Misri.

  4. Hosea 11:2takriban 740 KK

    Lakini kadiri nilivyomwita Israeli, ndivyo walivyokwenda mbali nami. Walitoa dhabihu kwa Mabaali na kufukiza uvumba kwa vinyago.

  5. Hosea 11:3takriban 740 KK

    Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea, nikiwashika mikono; lakini hawakutambua kuwa ni mimi niliyewaponya.

  6. Hosea 11:4takriban 740 KK

    Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu, kwa vifungo vya upendo; niliondoa nira shingoni mwao nami nikainama kuwalisha.

  7. Hosea 11:5takriban 740 KK

    “Je, hawatarudi Misri, nayo Ashuru haitawatawala kwa sababu wamekataa kutubu?

  8. Hosea 11:6takriban 740 KK

    Panga zitametameta katika miji yao, zitaharibu makomeo ya malango yao na kukomesha mipango yao.

  9. Hosea 11:7takriban 740 KK

    Watu wangu wamedhamiria kuniacha. Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana, kwa vyovyote hatawainua.

  10. Hosea 11:8takriban 740 KK

    “Efraimu, ninawezaje kukuacha? Ee Israeli, ninawezaje kukutoa? Nitawezaje kukutendea kama Adma? Nitawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zote zimeamshwa.

  11. Hosea 11:9takriban 740 KK

    Sitatimiza hasira yangu kali, wala sitageuka na kumharibu Efraimu. Kwa kuwa mimi ndimi Mungu, wala si mwanadamu, Aliye Mtakatifu miongoni mwenu. Sitakuja kwa ghadhabu.

  12. Hosea 11:10takriban 740 KK

    Watamfuata Bwana; atanguruma kama simba. Wakati angurumapo, watoto wake watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.

  13. Hosea 11:11takriban 740 KK

    Watakuja wakitetemeka kama ndege wakitoka Misri, kama hua wakitoka Ashuru. Nitawakalisha katika nyumba zao,” asema Bwana.

  14. Hosea 11:12takriban 740 KK

    Efraimu amenizunguka kwa uongo, nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu, hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

  15. Hosea 12:1takriban 725 KK

    Efraimu anajilisha upepo; hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima na kuzidisha uongo na jeuri. Anafanya mkataba na Ashuru na kutuma mafuta ya zeituni Misri.

  16. Hosea 12:2takriban 725 KK

    Bwana analo shtaka dhidi ya Yuda, atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.

  17. Hosea 12:3takriban 725 KK

    Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake; kama mwanadamu, alishindana na Mungu.

  18. Hosea 12:4takriban 725 KK

    Alishindana na malaika na kumshinda; alilia na kuomba upendeleo wake. Alimkuta huko Betheli na kuzungumza naye huko:

  19. Hosea 12:5takriban 725 KK

    Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Bwana ndilo jina lake!

  20. Hosea 12:6takriban 725 KK

    Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako; dumisha upendo na haki, nawe umngojee Mungu wako siku zote.

  21. Hosea 12:7takriban 725 KK

    Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu; hupenda kupunja.

  22. Hosea 12:8takriban 725 KK

    Efraimu hujisifu akisema, “Mimi ni tajiri sana; nimetajirika. Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu uovu wowote au dhambi.”

  23. Hosea 12:9takriban 725 KK

    “Mimi ndimi Bwana Mungu wenu niliyewaleta kutoka Misri; nitawafanya mkae tena kwenye mahema, kama vile katika siku za sikukuu zenu zilizoamriwa.

  24. Hosea 12:10takriban 725 KK

    Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi na kusema mifano kupitia wao.”

  25. Hosea 12:11takriban 725 KK

    Je, Gileadi si mwovu? Watu wake hawafai kitu! Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali? Madhabahu zao zitakuwa kama malundo ya mawe katika shamba lililolimwa.