Rukia maudhui

circa 1446 BC

Sinai & The Law

God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.

1,657 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Walawi 14:37takriban 1490 KK

    Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,

  2. Walawi 14:38takriban 1490 KK

    kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.

  3. Walawi 14:39takriban 1490 KK

    Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,

  4. Walawi 14:40takriban 1490 KK

    ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.

  5. Walawi 14:41takriban 1490 KK

    Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.

  6. Walawi 14:42takriban 1490 KK

    Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.

  7. Walawi 14:43takriban 1490 KK

    “Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,

  8. Walawi 14:44takriban 1490 KK

    kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.

  9. Walawi 14:45takriban 1490 KK

    Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.

  10. Walawi 14:46takriban 1490 KK

    “Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.

  11. Walawi 14:47takriban 1490 KK

    Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.

  12. Walawi 14:48takriban 1490 KK

    “Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.

  13. Walawi 14:49takriban 1490 KK

    Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.

  14. Walawi 14:50takriban 1490 KK

    Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.

  15. Walawi 14:51takriban 1490 KK

    Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.

  16. Walawi 14:52takriban 1490 KK

    Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.

  17. Walawi 14:53takriban 1490 KK

    Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”

  18. Walawi 14:54takriban 1490 KK

    Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,

  19. Walawi 14:55takriban 1490 KK

    upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,

  20. Walawi 14:56takriban 1490 KK

    kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,

  21. Walawi 14:57takriban 1490 KK

    kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

  22. Walawi 15:1takriban 1490 KK

    Bwana akawaambia Mose na Aroni,

  23. Walawi 15:2takriban 1490 KK

    “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.

  24. Walawi 15:3takriban 1490 KK

    Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:

  25. Walawi 15:4takriban 1490 KK

    “ ‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi.