- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- 2 Wakorintho 3:15takriban 60 BK
Hata leo Sheria ya Mose inaposomwa, utaji hufunika mioyo yao.
- 2 Wakorintho 3:16takriban 60 BK
Lakini wakati wowote mtu anapomgeukia Bwana, utaji unaondolewa.
- 2 Wakorintho 3:17takriban 60 BK
Basi Bwana ndiye Roho. Mahali alipo Roho wa Bwana hapo pana uhuru.
- 2 Wakorintho 3:18takriban 60 BK
Nasi sote, tukiwa na nyuso zisizotiwa utaji tunadhihirisha utukufu wa Bwana, kama kwenye kioo. Nasi tunabadilishwa ili tufanane naye, toka utukufu hadi utukufu mkuu zaidi, utokao kwa Bwana, ambaye ndiye Roho.
- 2 Wakorintho 4:1takriban 60 BK
Kwa hiyo, kwa kuwa tuna huduma hii kwa rehema za Mungu, hatukati tamaa.
- 2 Wakorintho 4:2takriban 60 BK
Tumekataa mambo ya siri na ya aibu, wala hatufuati njia za udanganyifu, tukichanganya Neno la Mungu na uongo. Kinyume cha hayo, tunadhihirisha kweli waziwazi na kujitambulisha wenyewe kwenye dhamiri ya kila mtu mbele za Mungu.
- 2 Wakorintho 4:3takriban 60 BK
Hata nayo Injili yetu kama imetiwa utaji, ni kwa wale tu wanaopotea.
- 2 Wakorintho 4:4takriban 60 BK
Kwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu.
- 2 Wakorintho 4:5takriban 60 BK
Kwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhubiri Yesu Kristo kuwa ni Bwana na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
- 2 Wakorintho 4:6takriban 60 BK
Kwa kuwa Mungu, yeye aliyesema, “Nuru na ingʼae gizani,” ameifanya nuru yake ingʼae mioyoni mwetu ili kutupatia nuru ya maarifa ya utukufu wa Mungu katika uso wa Kristo.
- 2 Wakorintho 4:7takriban 60 BK
Lakini tunayo hazina hii katika vyombo vya udongo, ili ijulikane wazi kwamba uwezo huu wa ajabu unatoka kwa Mungu wala si kwetu.
- 2 Wakorintho 4:8takriban 60 BK
Twataabika kila upande lakini hatuangamizwi; twaona wasiwasi lakini hatukati tamaa;
- 2 Wakorintho 4:9takriban 60 BK
twateswa lakini hatuachwi; twatupwa chini lakini hatupondwi.
- 2 Wakorintho 4:10takriban 60 BK
Siku zote twachukua katika mwili kufa kwake Yesu ili kwamba uzima wa Yesu uweze kudhihirika katika miili yetu.
- 2 Wakorintho 4:11takriban 60 BK
Kwa maana sisi tulio hai siku zote tumetolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili kwamba uzima wake upate kudhihirishwa katika mwili wetu upatikanao na mauti.
- 2 Wakorintho 4:12takriban 60 BK
Hivyo basi, mauti inatenda kazi ndani yetu, bali uzima unatenda kazi ndani yenu.
- 2 Wakorintho 4:13takriban 60 BK
Imeandikwa, “Niliamini, kwa hiyo nimesema.” Kwa roho yule yule wa imani pia tuliamini na hivyo tunasema,
- 2 Wakorintho 4:14takriban 60 BK
kwa sababu tunajua kwamba yeye aliyemfufua Bwana Yesu kutoka kwa wafu, atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuleta sisi pamoja nanyi mbele zake.
- 2 Wakorintho 4:15takriban 60 BK
Haya yote ni kwa faida yenu, ili kwamba neema ile inavyowafikia watu wengi zaidi na zaidi, ipate kusababisha shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
- 2 Wakorintho 4:16takriban 60 BK
Kwa hiyo, hatukati tamaa. Ingawa utu wetu wa nje unachakaa, utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
- 2 Wakorintho 4:17takriban 60 BK
Kwa maana dhiki yetu nyepesi iliyo ya kitambo inatutayarisha kwa ajili ya utukufu wa milele unaozidi kuwa mwingi kupita kiasi,
- 2 Wakorintho 4:18takriban 60 BK
kwa sababu hatuangalii yale yanayoweza kuonekana bali yale yasiyoweza kuonekana. Kwa maana yale yanayoweza kuonekana ni ya kitambo tu, bali yale yasiyoweza kuonekana ni ya milele.
- 2 Wakorintho 5:1takriban 60 BK
Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu.
- 2 Wakorintho 5:2takriban 60 BK
Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
- 2 Wakorintho 5:3takriban 60 BK
kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.