- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Sin (1)
Mistari muhimu ya Biblia
Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
Naungama uovu wangu, ninataabishwa na dhambi yangu.
Ee Bwana, usizuilie huruma zako, upendo wako na kweli yako daima vinilinde.
Kwa maana taabu zisizo na hesabu zimenizunguka, dhambi zangu zimenikamata, hata nisiweze kuona. Zimekuwa nyingi kuliko nywele za kichwa changu, nao moyo unazimia ndani yangu.
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
Unioshe na uovu wangu wote na unitakase dhambi yangu.
Kwa maana ninajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi na kufanya yaliyo mabaya machoni pako, ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo, na kuwa na haki utoapo hukumu.
Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi, mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu, wala hatia yangu haikufichika kwako.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; Bwana Mungu wetu atawaangamiza.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe; kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.
Atakufa kwa kukosa nidhamu, akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.