Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Resignation

132 mistari · 30 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Ndipo Ayubu akachukua kigae na kujikuna nacho huku akiketi kwenye majivu.

  2. Mke wake akamwambia, “Je, bado unashikamana na uadilifu wako? Mlaani Mungu nawe ukafe!”

  3. Akamjibu, “Unazungumza kama vile ambavyo mwanamke mpumbavu yeyote angenena. Je, tupokee mema mikononi mwa Mungu, nasi tusipokee na udhia?” Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi katika kusema kwake.

  4. “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.

  5. “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.

  6. Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.

  7. Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,

  8. kwa maana kama majani watanyauka mara, kama mimea ya kijani watakufa mara.

  9. Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.

  10. Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.

  11. Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:

  12. Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.

  13. Tulia mbele za Bwana na umngojee kwa uvumilivu; usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, wanapotekeleza mipango yao miovu.

  14. Epuka hasira na uache ghadhabu, usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.

  15. Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.

  16. Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.

  17. Bali wanyenyekevu watairithi nchi na wafurahie amani tele.

  18. Nilinyamaza kimya, sikufumbua kinywa changu, kwa sababu wewe ndiwe uliyetenda hili.

  19. Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka? Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu? Weka tumaini lako kwa Mungu, kwa sababu bado nitamsifu, Mwokozi wangu na

  20. Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka? Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu? Weka tumaini lako kwa Mungu, kwa sababu bado nitamsifu, Mwokozi wangu na Mungu wangu.

  21. “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”

  22. yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.

  23. Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.

  24. Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,

  25. Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?