Mistari ya Biblia kuhusu Paul: Revisits Pisidia, Pamphylia, Perga, Attalia, and Antioch, in Syria, where he abode
Mistari kuhusu Revisits Pisidia, Pamphylia, Perga, Attalia, and Antioch, in Syria, where he abode
Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.