Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 12:15takriban 33 BK

    “Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”

  2. Yohana 12:16takriban 33 BK

    Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.

  3. Yohana 12:17takriban 33 BK

    Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.

  4. Yohana 12:18takriban 33 BK

    Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.

  5. Yohana 12:19takriban 33 BK

    Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”

  6. Yohana 12:20takriban 33 BK

    Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.

  7. Yohana 12:21takriban 33 BK

    Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”

  8. Yohana 12:22takriban 33 BK

    Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.

  9. Yohana 12:23takriban 33 BK

    Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.

  10. Yohana 12:24takriban 33 BK

    Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.

  11. Yohana 12:25takriban 33 BK

    Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele.

  12. Yohana 12:26takriban 33 BK

    Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.

  13. Yohana 12:27takriban 33 BK

    “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.

  14. Yohana 12:28takriban 33 BK

    Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”

  15. Yohana 12:29takriban 33 BK

    Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”

  16. Yohana 12:30takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.

  17. Yohana 12:31takriban 33 BK

    Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.

  18. Yohana 12:32takriban 33 BK

    Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”

  19. Yohana 12:33takriban 33 BK

    Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.

  20. Yohana 12:34takriban 33 BK

    Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?”

  21. Yohana 12:35takriban 33 BK

    Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.

  22. Yohana 12:36takriban 33 BK

    Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.

  23. Yohana 12:37takriban 33 BK

    Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.

  24. Yohana 12:38takriban 33 BK

    Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”

  25. Yohana 12:39takriban 33 BK

    Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine: