circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Yohana 11:22takriban 33 BK
Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
- Yohana 11:23takriban 33 BK
Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
- Yohana 11:24takriban 33 BK
Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
- Yohana 11:25takriban 33 BK
Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
- Yohana 11:26takriban 33 BK
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?”
- Yohana 11:27takriban 33 BK
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
- Yohana 11:28takriban 33 BK
Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
- Yohana 11:29takriban 33 BK
Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
- Yohana 11:30takriban 33 BK
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
- Yohana 11:31takriban 33 BK
Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
- Yohana 11:32takriban 33 BK
Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
- Yohana 11:33takriban 33 BK
Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
- Yohana 11:34takriban 33 BK
Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
- Yohana 11:35takriban 33 BK
Yesu akalia machozi.
- Yohana 11:36takriban 33 BK
Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
- Yohana 11:37takriban 33 BK
Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
- Yohana 11:38takriban 33 BK
Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
- Yohana 11:39takriban 33 BK
Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
- Yohana 11:40takriban 33 BK
Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
- Yohana 11:41takriban 33 BK
Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
- Yohana 11:42takriban 33 BK
Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
- Yohana 11:43takriban 33 BK
Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
- Yohana 11:44takriban 33 BK
Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
- Yohana 11:45takriban 33 BK
Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
- Yohana 11:46takriban 33 BK
Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.