Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 11:22takriban 33 BK

    Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”

  2. Yohana 11:23takriban 33 BK

    Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”

  3. Yohana 11:24takriban 33 BK

    Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”

  4. Yohana 11:25takriban 33 BK

    Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi

  5. Yohana 11:26takriban 33 BK

    na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?”

  6. Yohana 11:27takriban 33 BK

    Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”

  7. Yohana 11:28takriban 33 BK

    Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”

  8. Yohana 11:29takriban 33 BK

    Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.

  9. Yohana 11:30takriban 33 BK

    Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.

  10. Yohana 11:31takriban 33 BK

    Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.

  11. Yohana 11:32takriban 33 BK

    Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”

  12. Yohana 11:33takriban 33 BK

    Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.

  13. Yohana 11:34takriban 33 BK

    Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”

  14. Yohana 11:35takriban 33 BK

    Yesu akalia machozi.

  15. Yohana 11:36takriban 33 BK

    Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”

  16. Yohana 11:37takriban 33 BK

    Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”

  17. Yohana 11:38takriban 33 BK

    Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.

  18. Yohana 11:39takriban 33 BK

    Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”

  19. Yohana 11:40takriban 33 BK

    Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”

  20. Yohana 11:41takriban 33 BK

    Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.

  21. Yohana 11:42takriban 33 BK

    Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”

  22. Yohana 11:43takriban 33 BK

    Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”

  23. Yohana 11:44takriban 33 BK

    Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”

  24. Yohana 11:45takriban 33 BK

    Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.

  25. Yohana 11:46takriban 33 BK

    Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.