Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 10:39takriban 33 BK

    Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.

  2. Yohana 10:40takriban 33 BK

    Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.

  3. Yohana 10:41takriban 33 BK

    Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”

  4. Yohana 10:42takriban 33 BK

    Nao wengi wakamwamini Yesu huko.

  5. Yohana 11:1takriban 33 BK

    Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.

  6. Yohana 11:2takriban 33 BK

    Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.

  7. Yohana 11:3takriban 33 BK

    Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”

  8. Yohana 11:4takriban 33 BK

    Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”

  9. Yohana 11:5takriban 33 BK

    Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,

  10. Yohana 11:6takriban 33 BK

    baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.

  11. Yohana 11:7takriban 33 BK

    Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”

  12. Yohana 11:8takriban 33 BK

    Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”

  13. Yohana 11:9takriban 33 BK

    Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.

  14. Yohana 11:10takriban 33 BK

    Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”

  15. Yohana 11:11takriban 33 BK

    Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”

  16. Yohana 11:12takriban 33 BK

    Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”

  17. Yohana 11:13takriban 33 BK

    Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.

  18. Yohana 11:14takriban 33 BK

    Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.

  19. Yohana 11:15takriban 33 BK

    Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”

  20. Yohana 11:16takriban 33 BK

    Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”

  21. Yohana 11:17takriban 33 BK

    Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.

  22. Yohana 11:18takriban 33 BK

    Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,

  23. Yohana 11:19takriban 33 BK

    na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.

  24. Yohana 11:20takriban 33 BK

    Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.

  25. Yohana 11:21takriban 33 BK

    Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.