circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Yohana 10:39takriban 33 BK
Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
- Yohana 10:40takriban 33 BK
Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
- Yohana 10:41takriban 33 BK
Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
- Yohana 10:42takriban 33 BK
Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
- Yohana 11:1takriban 33 BK
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
- Yohana 11:2takriban 33 BK
Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
- Yohana 11:3takriban 33 BK
Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
- Yohana 11:4takriban 33 BK
Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
- Yohana 11:5takriban 33 BK
Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
- Yohana 11:6takriban 33 BK
baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
- Yohana 11:7takriban 33 BK
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
- Yohana 11:8takriban 33 BK
Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
- Yohana 11:9takriban 33 BK
Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
- Yohana 11:10takriban 33 BK
Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
- Yohana 11:11takriban 33 BK
Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
- Yohana 11:12takriban 33 BK
Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
- Yohana 11:13takriban 33 BK
Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
- Yohana 11:14takriban 33 BK
Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
- Yohana 11:15takriban 33 BK
Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
- Yohana 11:16takriban 33 BK
Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
- Yohana 11:17takriban 33 BK
Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
- Yohana 11:18takriban 33 BK
Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
- Yohana 11:19takriban 33 BK
na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
- Yohana 11:20takriban 33 BK
Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
- Yohana 11:21takriban 33 BK
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.