Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 9:30takriban 33 BK

    Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!

  2. Yohana 9:31takriban 33 BK

    Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.

  3. Yohana 9:32takriban 33 BK

    Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu.

  4. Yohana 9:33takriban 33 BK

    Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”

  5. Yohana 9:34takriban 33 BK

    Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.

  6. Yohana 9:35takriban 33 BK

    Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”

  7. Yohana 9:36takriban 33 BK

    Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”

  8. Yohana 9:37takriban 33 BK

    Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”

  9. Yohana 9:38takriban 33 BK

    Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.

  10. Yohana 9:39takriban 33 BK

    Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”

  11. Yohana 9:40takriban 33 BK

    Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”

  12. Yohana 9:41takriban 33 BK

    Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.

  13. Yohana 10:1takriban 33 BK

    “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.

  14. Yohana 10:2takriban 33 BK

    Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.

  15. Yohana 10:3takriban 33 BK

    Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.

  16. Yohana 10:4takriban 33 BK

    Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.

  17. Yohana 10:5takriban 33 BK

    Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”

  18. Yohana 10:6takriban 33 BK

    Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.

  19. Yohana 10:7takriban 33 BK

    Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.

  20. Yohana 10:8takriban 33 BK

    Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.

  21. Yohana 10:9takriban 33 BK

    Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.

  22. Yohana 10:10takriban 33 BK

    Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.

  23. Yohana 10:11takriban 33 BK

    “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.

  24. Yohana 10:12takriban 33 BK

    Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.

  25. Yohana 10:13takriban 33 BK

    Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.