circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Yohana 9:30takriban 33 BK
Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
- Yohana 9:31takriban 33 BK
Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
- Yohana 9:32takriban 33 BK
Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu.
- Yohana 9:33takriban 33 BK
Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
- Yohana 9:34takriban 33 BK
Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
- Yohana 9:35takriban 33 BK
Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
- Yohana 9:36takriban 33 BK
Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
- Yohana 9:37takriban 33 BK
Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
- Yohana 9:38takriban 33 BK
Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
- Yohana 9:39takriban 33 BK
Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
- Yohana 9:40takriban 33 BK
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
- Yohana 9:41takriban 33 BK
Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.
- Yohana 10:1takriban 33 BK
“Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
- Yohana 10:2takriban 33 BK
Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
- Yohana 10:3takriban 33 BK
Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
- Yohana 10:4takriban 33 BK
Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
- Yohana 10:5takriban 33 BK
Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
- Yohana 10:6takriban 33 BK
Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
- Yohana 10:7takriban 33 BK
Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
- Yohana 10:8takriban 33 BK
Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
- Yohana 10:9takriban 33 BK
Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
- Yohana 10:10takriban 33 BK
Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
- Yohana 10:11takriban 33 BK
“Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
- Yohana 10:12takriban 33 BK
Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
- Yohana 10:13takriban 33 BK
Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.