Rukia maudhui

circa 1446 BC

Sinai & The Law

God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.

1,657 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Walawi 7:19takriban 1490 KK

    “ ‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.

  2. Walawi 7:20takriban 1490 KK

    Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.

  3. Walawi 7:21takriban 1490 KK

    Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’ ”

  4. Walawi 7:22takriban 1490 KK

    Bwana akamwambia Mose,

  5. Walawi 7:23takriban 1490 KK

    “Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.

  6. Walawi 7:24takriban 1490 KK

    Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.

  7. Walawi 7:25takriban 1490 KK

    Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.

  8. Walawi 7:26takriban 1490 KK

    Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.

  9. Walawi 7:27takriban 1490 KK

    Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’ ”

  10. Walawi 7:28takriban 1490 KK

    Bwana akamwambia Mose,

  11. Walawi 7:29takriban 1490 KK

    “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.

  12. Walawi 7:30takriban 1490 KK

    Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.

  13. Walawi 7:31takriban 1490 KK

    Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.

  14. Walawi 7:32takriban 1490 KK

    Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.

  15. Walawi 7:33takriban 1490 KK

    Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.

  16. Walawi 7:34takriban 1490 KK

    Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’ ”

  17. Walawi 7:35takriban 1490 KK

    Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.

  18. Walawi 7:36takriban 1490 KK

    Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.

  19. Walawi 7:37takriban 1490 KK

    Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,

  20. Walawi 7:38takriban 1490 KK

    ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.

  21. Walawi 8:1takriban 1490 KK

    Bwana akamwambia Mose,

  22. Walawi 8:2takriban 1490 KK

    “Waletee Aroni na wanawe mavazi yao, mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili na kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu.

  23. Walawi 8:3takriban 1490 KK

    Kisha kusanya mkutano wote kwenye ingilio la Hema la Kukutania.”

  24. Walawi 8:4takriban 1490 KK

    Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza, na mkutano ukakusanyika kwenye ingilio la Hema la Kukutania.

  25. Walawi 8:5takriban 1490 KK

    Mose akaliambia kusanyiko, “Hili ndilo Bwana ameagiza lifanyike.”