Rukia maudhui

circa 2100–1900 BC

Abraham: The Covenant

God calls Abram from Ur, establishes an everlasting covenant, and promises a son through whom all nations will be blessed.

394 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Mwanzo 17:2takriban 1897 KK

    Nami nitafanya Agano langu kati yangu na wewe, nami nitakuzidisha sana sana.”

  2. Mwanzo 17:3takriban 1897 KK

    Abramu akaanguka kifudifudi, naye Mungu akamwambia,

  3. Mwanzo 17:4takriban 1897 KK

    “Kwa upande wangu, hili ndilo Agano langu na wewe: Wewe utakuwa baba wa mataifa mengi.

  4. Mwanzo 17:5takriban 1897 KK

    Jina lako hutaitwa tena Abramu, bali jina lako litakuwa Abrahamu, kwa maana nimekufanya wewe baba wa mataifa mengi.

  5. Mwanzo 17:6takriban 1897 KK

    Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, kwako yatatoka mataifa nao wafalme watatoka kwako.

  6. Mwanzo 17:7takriban 1897 KK

    Nitalithibitisha Agano langu kama Agano la milele kati yangu na wewe na wazao wako baada yako na vizazi vijavyo niwe Mungu wako na Mungu wa wazao wako.

  7. Mwanzo 17:8takriban 1897 KK

    Nchi yote ya Kanaani, unakoishi sasa kama mgeni, nitakupa kuwa milki yako milele, na uzao wako, nami nitakuwa Mungu wao.”

  8. Mwanzo 17:9takriban 1897 KK

    Ndipo Mungu akamwambia Abrahamu, “Kwa upande wako, lazima ushike Agano langu, wewe na wazao wako kwa ajili ya vizazi vijavyo.

  9. Mwanzo 17:10takriban 1897 KK

    Hili ni Agano langu na wewe pamoja na wazao wako baada yako, Agano mtakalolishika: Kila mwanaume miongoni mwenu atatahiriwa.

  10. Mwanzo 17:11takriban 1897 KK

    Mtafanyiwa tohara na hii itakuwa ni alama ya Agano kati yangu na ninyi.

  11. Mwanzo 17:12takriban 1897 KK

    Kwa vizazi vijavyo, kila mwanaume miongoni mwenu mwenye siku nane ni lazima atahiriwe, pamoja na watakaozaliwa nyumbani mwako au walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni, wale ambao sio watoto wako.

  12. Mwanzo 17:13takriban 1897 KK

    Awe amezaliwa nyumbani mwako au amenunuliwa kwa fedha yako, ni lazima watahiriwe. Agano langu katika mwili wako litakuwa ni Agano la milele.

  13. Mwanzo 17:14takriban 1897 KK

    Kila mwanaume asiyetahiriwa, ambaye hajapata tohara ya mwilini, atatengwa na watu wake, amelivunja Agano langu.”

  14. Mwanzo 17:15takriban 1897 KK

    Pia Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa upande wa Sarai mkeo, hutamwita tena Sarai bali jina lake litakuwa Sara.

  15. Mwanzo 17:16takriban 1897 KK

    Nitambariki na hakika nitakupatia mwana kwake. Nitambariki na kwamba atakuwa mama wa mataifa, wafalme wa mataifa watatoka kwake.”

  16. Mwanzo 17:17takriban 1897 KK

    Abrahamu akaanguka kifudifudi, akacheka na kusema moyoni mwake, “Je, mtu wa miaka mia moja aweza kuzaa mwana? Je, Sara atazaa mtoto katika umri wa miaka tisini?”

  17. Mwanzo 17:18takriban 1897 KK

    Abrahamu akamwambia Mungu, “Laiti Ishmaeli naye angeshiriki baraka yako!”

  18. Mwanzo 17:19takriban 1897 KK

    Ndipo Mungu akasema, “Ndiyo, lakini mkeo Sara atakuzalia wewe mwana, nawe utamwita jina lake Isaki. Nitalithibitisha Agano langu naye kama Agano la milele kwa ajili yake na wazao wake baada yake.

  19. Mwanzo 17:20takriban 1897 KK

    Kwa upande wa Ishmaeli, nimekusikia: hakika nitambariki, nitamfanya awe na uzao mwingi na nitaongeza sana idadi yake. Atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kubwa.

  20. Mwanzo 17:21takriban 1897 KK

    Lakini Agano langu nitalithibitisha kwa Isaki, ambaye Sara atakuzalia mwaka ujao majira kama haya.”

  21. Mwanzo 17:22takriban 1897 KK

    Wakati alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, Mungu akapanda juu akaondoka kwa Abrahamu.

  22. Mwanzo 17:23takriban 1897 KK

    Siku ile ile, Abrahamu akamchukua Ishmaeli mwanawe na wote waliozaliwa nyumbani mwake pamoja na walionunuliwa kwa fedha zake, kila mwanaume wa nyumbani mwake, akawatahiri, kama Mungu alivyomwagiza.

  23. Mwanzo 17:24takriban 1897 KK

    Abrahamu alikuwa na umri wa miaka tisini na tisa alipotahiriwa,

  24. Mwanzo 17:25takriban 1897 KK

    naye Ishmaeli mwanawe alitahiriwa akiwa na umri wa miaka kumi na mitatu.

  25. Mwanzo 17:26takriban 1897 KK

    Abrahamu na Ishmaeli mwanawe walitahiriwa siku ile ile,