God
Mistari inayomtaja God
Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
“Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili nami ni safi mbele zako.’
Aha! Laiti kwamba Mungu angesema, kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,
naye akufunulie siri za hekima, kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili. Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.
“Je, waweza kujua siri za Mungu? Je, waweza kuyachunguza mambo yote kumhusu Mwenyezi?
“Kama akija na kukufunga gerezani, na kuitisha mahakama, ni nani awezaye kumpinga?
Hakika anawatambua watu wadanganyifu; naye aonapo uovu, je, haangalii?
“Hata sasa ukiutoa moyo wako kwake na kumwinulia mikono yako,
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.