Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Instruction

179 mistari · 2 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.

  2. Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.

  3. Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.

  4. Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,

  5. kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.

  6. Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.

  7. Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.

  8. Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.

  9. Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.

  10. Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.

  11. Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.

  12. Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.

  13. Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako.

  14. Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.

  15. Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.

  16. Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.

  17. Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.

  18. Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.

  19. Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.

  20. Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.

  21. Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.

  22. Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.

  23. Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.

  24. Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.

  25. Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.