- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Instruction
Mistari muhimu ya Biblia
Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako.
Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa juu ya sheria zako wakati wote.
Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.
Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako.
Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu.
Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.
Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana, usiniache niaibishwe.
Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.
Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho.
Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote.
Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha.
Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa.
Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema.
Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.