- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Instruction
Mistari muhimu ya Biblia
Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.