- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Instruction
Mistari muhimu ya Biblia
Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako, kwa maana udanganyifu wao ni bure.
Waovu wa nchi unawatupa kama takataka, kwa hivyo nazipenda sheria zako.
Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe, ninaziogopa sheria zako.
Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,