Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu God

662 mistari · 46 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.

  2. Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.

  3. “Naam, najua hili ni kweli. Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?

  4. Ingawa mtu angetaka kushindana naye, asingaliweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja.

  5. Hekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno. Ni nani aliyempinga naye akawa salama?

  6. Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.

  7. Aitikisa dunia kutoka mahali pake na kuzifanya nguzo zake zitetemeke.

  8. Husema na jua, nalo likaacha kuangaza; naye huizima mianga ya nyota.

  9. Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

  10. Yeye ndiye Muumba wa nyota za Dubu, na Orioni, Kilimia, na makundi ya nyota za kusini.

  11. Hutenda maajabu yasiyopimika, miujiza isiyoweza kuhesabiwa.

  12. Anapopita karibu nami, siwezi kumwona; apitapo mbele yangu, simtambui.

  13. Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’

  14. Mungu hataizuia hasira yake; hata jeshi kubwa la Rahabu lenye nguvu linajikunyata miguuni pake.

  15. “Ni vipi basi mimi nitaweza kubishana naye? Nawezaje kupata maneno ya kuhojiana naye?

  16. Ingawa sikuwa na hatia, sikuweza kumjibu; ningeweza tu kumsihi Mhukumu wangu anihurumie.

  17. Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, siamini kama angenisikiliza.

  18. Yeye angeniangamiza kwa dhoruba na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu.

  19. Asingeniacha nipumue bali angenifunika kabisa na huzuni kuu.

  20. Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani?

  21. Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.

  22. “Ingawa mimi sina kosa, haileti tofauti katika nafsi yangu; nauchukia uhai wangu.

  23. Hayo yote ni sawa; ndiyo sababu nasema, ‘Yeye huwaangamiza wasio na makosa pamoja na waovu.’

  24. Wakati pigo liletapo kifo cha ghafula, yeye hudhihaki kule kukata tamaa kwa yule asiye na kosa.

  25. Wakati nchi inapoangukia mikononi mwa waovu, yeye huwafunga macho mahakimu wake. Kama si yeye, basi ni nani?