- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Company
Mistari muhimu ya Biblia
Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira ya haraka, usishirikiane na yule aliye mwepesi kukasirika,
la sivyo utajifunza njia zake na kujiingiza mwenyewe kwenye mtego.
Bwana alisema nami mkono wake wenye nguvu ukiwa juu yangu, akinionya nisifuate njia za taifa hili. Akasema:
“Usiite fitina kila kitu ambacho watu hawa hukiita fitina, usiogope kile wanachokiogopa, wala usikihofu.
“Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.